إِنَّمَا يَفۡتَرِي ٱلۡكَذِبَ ٱلَّذِينَ لَا يُؤۡمِنُونَ بِـَٔايَٰتِ ٱللَّهِۖ وَأُوْلَـٰٓئِكَ هُمُ ٱلۡكَٰذِبُونَ
Wanao zua uwongo ni wale tu wasio ziamini Ishara za Mwenyezi Mungu. Na hao ndio waongo.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Kwa hakika wanaozua urongo ni wale wasiomuamini Mwenyezi Mungu na aya Zake, na wao ndio warongo kwa neno lao hilo. Ama Muhammad, rehema ya Mwenyezi Mungu na amani zimshukiye, anayemuamini Mola wake na kumnyenyekea, haiwezekani kwake yeye kumkanusha Mwenyezi Mungu na kumsingizia Asiyoyasema.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس