وَٱلۡأَنۡعَٰمَ خَلَقَهَاۖ لَكُمۡ فِيهَا دِفۡءٞ وَمَنَٰفِعُ وَمِنۡهَا تَأۡكُلُونَ
Na nyama hoa amekuumbieni. Katika hao mna vifaa vya kutia joto, na manufaa mengineyo, na baadhi yao mnawala.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Na wanyama miongoni mwa ngamia, ng’ombe na mbuzi, Mwenyezi Mungu Amewaumbia, enyi watu, na akajaalia joto katika sufi na manyoa yake, na manufaa mengine katika maziwa yake na ngozi zake na kuwatumia kwa kuwapanda na, wengine miongoni mwao, kuwala.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس