وَأَوۡحَىٰ رَبُّكَ إِلَى ٱلنَّحۡلِ أَنِ ٱتَّخِذِي مِنَ ٱلۡجِبَالِ بُيُوتٗا وَمِنَ ٱلشَّجَرِ وَمِمَّا يَعۡرِشُونَ
Na Mola wako Mlezi amemfunulia nyuki: Jitengenezee majumba yako katika milima, na katika miti, na katika wanayo jenga watu.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Na Mola wako, ewe Mtume, Aliwapa nyuki ufunzi kwamba jifanyieni nyumba kwenye majabali, kwenye miti na kwenye nyumba na sakafu zinazojengwa na watu.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس