ذُرِّيَّةَ مَنۡ حَمَلۡنَا مَعَ نُوحٍۚ إِنَّهُۥ كَانَ عَبۡدٗا شَكُورٗا
Enyi kizazi tuliyo wachukua pamoja na Nuhu! Hakika yeye alikuwa mja mwenye shukrani.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Enyi kizazi cha wale tuliowaokoa na tukawabeba pamoja na Nūḥ katika jahazi, msimshirikishe Mwenyezi Mungu katika kumuabudu, na kuweni ni wenye kushukuru neema Zake na ni wenye kumfuata Nūḥ, amani imshukiye, kwani yeye alikuwa ni mja mwenye kumshukuru Mwenyezi Mungu kwa moyo wake, ulimi wake na viungo vyake.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس