Al-Furkan
تَبَارَكَ ٱلَّذِي نَزَّلَ ٱلۡفُرۡقَانَ عَلَىٰ عَبۡدِهِۦ لِيَكُونَ لِلۡعَٰلَمِينَ نَذِيرًا
Ametukuka aliye teremsha Furqani kwa mja wake, ili awe mwonyaji kwa walimwengu wote.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Ni kubwa mno baraka za Mwenyezi Mungu na ni mengi sana mema Yake na ni kamilifu sifa Zake, Aliyetakasika na kutukuka, Ambaye Ameiteremsha Qur’ani, yenye kupambanua baina ya ukweli na ubatilifu, kwa mja Wake Muhammad, rehemea ya Mwenyezi Mungu na amani zimshukie, ili awe ni mjumbe kwa binadamu na majini na awe muonyaji wa adhabu ya Mwenyezi Mungu kwao.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس