وَإِنَّ كُلّٗا لَّمَّا لَيُوَفِّيَنَّهُمۡ رَبُّكَ أَعۡمَٰلَهُمۡۚ إِنَّهُۥ بِمَا يَعۡمَلُونَ خَبِيرٞ
Na hakika Mola wako Mlezi atawatimilizia malipo ya vitendo vyao. Hakika Yeye anayo khabari ya wayatendayo.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Na hakika watu wote hao wanaotafautiana tuliokutajia habari zao , ewe Mtume, Mwenyezi Mungu Atawatekelezea malipo ya matendo yao Siku ya Kiyama, yakiwa mema watalipwa wema na yakiwa maovu watalipwa uovu. Hakika Mola wako , kwa wanayoyafanya hawa washirikina, ni Mtambuzi, hakuna kitendo chao chochote kinachofichamana Kwake. Katika hii pana kitisho na onyo kwao.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس