وَمَا كَانَ رَبُّكَ لِيُهۡلِكَ ٱلۡقُرَىٰ بِظُلۡمٖ وَأَهۡلُهَا مُصۡلِحُونَ
Wala hakuwa Mola wako Mlezi wa kuihiliki miji kwa dhulma tu na hali watu wake ni watenda mema.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Na hakuwa Mola wako, ewe Mtume, ni Mwenye kuuangamiza mji wowote miongoni mwa miji na hali watu wake ni wenye kufanya mambo mazuri katika ardhi, wenye kujiepusha na uharibifu na udhalimu; Yeye huwaangamiza wao kwa sababu ya udhalimu wao na uharibifu wao.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس