فَلَمَّا ذَهَبَ عَنۡ إِبۡرَٰهِيمَ ٱلرَّوۡعُ وَجَآءَتۡهُ ٱلۡبُشۡرَىٰ يُجَٰدِلُنَا فِي قَوۡمِ لُوطٍ
Basi khofu ilipo mwondoka Ibrahim, na ikawa ile bishara imemfikia, alianza kujadiliana nasi juu ya kaumu ya Lut'.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Ulipomuondokea Ibrāhīm uoga uliompata kwa wale wageni kutokula chakula, na ikamjia bishara njema ya Isḥāq na Ya’qūb, aliendelea kuwajadili Wajumbe wetu juu ya kile tulichowatuma cha kuwaadhibu watu wa Lūṭ na kuwaangamiza.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس