وَلَقَدۡ نَعۡلَمُ أَنَّهُمۡ يَقُولُونَ إِنَّمَا يُعَلِّمُهُۥ بَشَرٞۗ لِّسَانُ ٱلَّذِي يُلۡحِدُونَ إِلَيۡهِ أَعۡجَمِيّٞ وَهَٰذَا لِسَانٌ عَرَبِيّٞ مُّبِينٌ
Na Sisi hakika tunajua kwamba wanasema: Yuko mtu anaye mfundisha. Lugha ya huyo wanaye muelekezea ni ya kigeni, na hii ni lugha ya Kiarabu mbayana.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Na kwa hakika tunajua kuwa washirikina wanasema kwamba Nabii anapokea Qur’ani kutoka kwa kiumbe miongoni mwa wanadamu. Wamesema urongo! Kwani ulimi wa yule waliomsingizia kuwa amemfundisha Nabii, rehema na amani zimshukie, si wa Kiarabu usiyotasua, na hii Qur’ani ni kwa lugha ya Kiarabu, imefikia upeo wa ufafanuzi na ubainifu.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس