فَٱدۡخُلُوٓاْ أَبۡوَٰبَ جَهَنَّمَ خَٰلِدِينَ فِيهَاۖ فَلَبِئۡسَ مَثۡوَى ٱلۡمُتَكَبِّرِينَ
Basi ingieni milango ya Jahannamu, humo mdumu. Ni maovu mno makaazi ya wafanyao kiburi!
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Ingieni milango ya Jahanamu. Hamtotoka humo milele. Na mahali hapo ni paovu pa kukaa wenye kiburi waliokataa kumuamini Mwenyezi Mungu, kumuabudu Yeye Peke Yake na kumtii.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس