وَٱللَّهُ جَعَلَ لَكُم مِّمَّا خَلَقَ ظِلَٰلٗا وَجَعَلَ لَكُم مِّنَ ٱلۡجِبَالِ أَكۡنَٰنٗا وَجَعَلَ لَكُمۡ سَرَٰبِيلَ تَقِيكُمُ ٱلۡحَرَّ وَسَرَٰبِيلَ تَقِيكُم بَأۡسَكُمۡۚ كَذَٰلِكَ يُتِمُّ نِعۡمَتَهُۥ عَلَيۡكُمۡ لَعَلَّكُمۡ تُسۡلِمُونَ
Na Mwenyezi Mungu amekufanyieni vivuli katika vitu alivyo viumba, na amekufanyieni maskani milimani, na amekufanyieni nguo za kukingeni na joto, na nguo za kukingeni katika vita vyenu. Ndio hivyo anakutimizieni neema zake ili mpate kut'ii.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Na Mwenyezi Mungu Amewaptia miti na vinginevyo vya kuwaletea vivuli, na amewafanyia kwenye majabali na pango sehemu za kuhamia mnapohitajia, na Amewafanyia nguo kutokana na pamba na sufi na vinginevyo za kuwahifadhi na joto na baridi, na Amewaumbia chuma cha nyinyi kujikinga na silaha za kudunga za maadui wenu na madhara yao katika vita vyenu na wao. Kama vile Alivyowaneemesha kwa neema hizi, atawakamilishia neema Zake kwenu kwa kuwafafanulia wazi Dini ya haki, ili mjisalimishe kwa amri ya Mwenyezi Mungu, Peke Yake, na msimshirikishe na kitu chochote katika ibada Yake.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس