وَإِذَا رَءَا ٱلَّذِينَ أَشۡرَكُواْ شُرَكَآءَهُمۡ قَالُواْ رَبَّنَا هَـٰٓؤُلَآءِ شُرَكَآؤُنَا ٱلَّذِينَ كُنَّا نَدۡعُواْ مِن دُونِكَۖ فَأَلۡقَوۡاْ إِلَيۡهِمُ ٱلۡقَوۡلَ إِنَّكُمۡ لَكَٰذِبُونَ
Na walio shirikisha watakapo waona hao walio washirikisha na Mwenyezi Mungu, watasema: Mola wetu Mlezi! Hawa ndio washirikishwa wetu ambao tulikuwa tukiwaabudu badala yako. Ndipo wale watakapo watupia kauli: Hakika nyinyi ni waongo!
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Na wale waliokanusha watakapowaona Siku ya Kiyama waungu wao waliokuwa wakiwaabudu pamoja na MwenyeziMungu watasema, «Mola wetu! Hawa ndio washirika wetu tuliokuwa tukiwaabudu badala yako.» Hapo waungu hao watatamka kuwakanusha wale waliowaabudu na watasema, «Hakika nyinyi, enyi washirikina, ni warongo, mlipotufanya sisi ni washirika wa Mwenyezi Mungu na mkatuabudu pamoja na Yeye. Sisi hatukuwaamuru hilo, wala hatukudai kwamba sisi tunastahiki uungu, lawama ni juu yenu.»
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس