مَا عِندَكُمۡ يَنفَدُ وَمَا عِندَ ٱللَّهِ بَاقٖۗ وَلَنَجۡزِيَنَّ ٱلَّذِينَ صَبَرُوٓاْ أَجۡرَهُم بِأَحۡسَنِ مَا كَانُواْ يَعۡمَلُونَ
Mlivyo navyo vitakwisha na vilivyoko kwa Mwenyezi Mungu ndivyo vitakavyo bakia. Na kwa yakini Sisi tutawapa walio subiri ujira wao kwa bora ya waliyo kuwa wakiyatenda.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Hayo mliyonayo, miongoni mwa taka za kilimwengu, yataondoka na yale yaliyoko kwa Mwenyezi Mungu, ya riziki na thawabu, hayataondoka. Na wale waliohimili kubeba mazito ya Sheria waliyotakiwa wayabebe, miongoni mwayo ikiwa ni utekelezaji ahadi, tutawalipa malipo mazuri zaidi ya matendo yao mema: tutawapa zaidi kwa matendo yao madogo kama tutakavyowapa zaidi kwa matendo yao makubwa kwa ukarimu wetu.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس