ٱنظُرۡ كَيۡفَ ضَرَبُواْ لَكَ ٱلۡأَمۡثَالَ فَضَلُّواْ فَلَا يَسۡتَطِيعُونَ سَبِيلٗا
Tazama vipi wanavyo kupigia mifano. Basi wamepotea. Kwa hivyo hawawezi kuipata njia.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Fikiri, ewe Mtume, kwa kulionea ajabu neno lao kwamba Muhammad ni mchawi mshairi mwenye wazimu. Hivyo basi wamekiuka mpaka na wamepotoka na hawakuongokea njia ya haki na usawa.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس