أَفَأَمِنتُمۡ أَن يَخۡسِفَ بِكُمۡ جَانِبَ ٱلۡبَرِّ أَوۡ يُرۡسِلَ عَلَيۡكُمۡ حَاصِبٗا ثُمَّ لَا تَجِدُواْ لَكُمۡ وَكِيلًا
Je! Mmeaminisha ya kuwa hatakudidimizeni upande wowote katika nchi kavu, au kwamba hatakuleteeni tufani la kokoto? Kisha msipate wa kumtegemea.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Je, mumeghafilika, enyi watu, na adhabu ya Mwenyezi Mungu, ndipo mkajiaminisha kwamba ardhi haitawaporomokea ikawadidimiza au kwamba Mwenyezi Mungu Hatawanyesheza mvua ya mawe itokayo juu iwaue kisha msipate yoyote wa kuwalinda na adhabu Yake?
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس