وَقَالُواْ لَوۡلَا نُزِّلَ هَٰذَا ٱلۡقُرۡءَانُ عَلَىٰ رَجُلٖ مِّنَ ٱلۡقَرۡيَتَيۡنِ عَظِيمٍ
Na walisema: Kwa nini Qur'ani hii haikuteremshwa kwa mtu mkubwa katika miji miwili hii?
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Na hawa washirikina wa Kikureshi walisema, «Iwapo hii Qur’ani inatoka kwa Mwenyezi Mungu kikweli, basi si ateremshiwe mtu mkuu kutoka miji hii miwili: Makkah au Ṭāif.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس