وَإِنَّهُمۡ لَيَصُدُّونَهُمۡ عَنِ ٱلسَّبِيلِ وَيَحۡسَبُونَ أَنَّهُم مُّهۡتَدُونَ
Na hakika wao wanawazuilia Njia na wenyewe wanadhani kuwa wameongoka.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Na kwa hakika, Mashetani wanawazuia hawa wanaoupa mgongo utajo wa Mwenyezi Mungu wasifuate njia ya haki, wanawapambia upotevu na wanawafanya wachukie Kumuamini Mwenyezi Mungu na kufanya matendo ya utiifu Kwake. Na wanadhani hawa wenye kupa mgongo, kutokana na vile Mashetani wanavyowapambia upotevu walionao, wanadhani kuwa wao wako kwenye haki na uongofu.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس