هَلۡ يَنظُرُونَ إِلَّا ٱلسَّاعَةَ أَن تَأۡتِيَهُم بَغۡتَةٗ وَهُمۡ لَا يَشۡعُرُونَ
Je! Nini wanangojea ila Saa iwajie kwa ghafla na wala wao hawatambui?
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Je, kwani wana kutu chochote wanachokingojea watu wa makundi hayo waliotafautiana kuhusu Īsā isipokuwa ni kujiwa na Kiyama kwa ghafla na hali wao hawahisi wala hawatambui?
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس