ثُمَّ إِنَّ رَبَّكَ لِلَّذِينَ هَاجَرُواْ مِنۢ بَعۡدِ مَا فُتِنُواْ ثُمَّ جَٰهَدُواْ وَصَبَرُوٓاْ إِنَّ رَبَّكَ مِنۢ بَعۡدِهَا لَغَفُورٞ رَّحِيمٞ
Kisha hakika Mola wako Mlezi, kwa wale walio hama makwao baada ya kuteswa, kisha wakapigania Dini na wakasubiri, bila ya shaka Mola wako Mlezi baada ya hayo ni Mwenye kusamehe Mwenye kurehemu.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Kisha Mola wako, kwa wale waliofanywa wanyonge ndani ya Makkah na wakaadhibiwa na washirikina mpaka wakakubali matendo yao kijuujuu, wakawafitini kwa kutamka yanayowaridhi, na hali nyoyo zao zimetulia katika Imani, na ilipowezekana kwao kujiokoa waligura kwenda Madina kisha wakapigana jihadi katika njia ya Mwenyezi Mungu na wakavumilia mashaka ya majukumu, hakika Mola wako , baada ya kutubia kwao ni Mwenye kuwasamehe , ni Mwenye kuwarehemu.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس