۞وَقِيلَ لِلَّذِينَ ٱتَّقَوۡاْ مَاذَآ أَنزَلَ رَبُّكُمۡۚ قَالُواْ خَيۡرٗاۗ لِّلَّذِينَ أَحۡسَنُواْ فِي هَٰذِهِ ٱلدُّنۡيَا حَسَنَةٞۚ وَلَدَارُ ٱلۡأٓخِرَةِ خَيۡرٞۚ وَلَنِعۡمَ دَارُ ٱلۡمُتَّقِينَ
Na wataambiwa walio mcha Mungu: Mola wenu Mlezi kateremsha nini? Watasema: Kheri. Walio fanya wema katika dunia hii watapata wema. Na nyumba ya Akhera ni bora zaidi, na njema mno nyumba ya wachamngu.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Na wanapoambiwa Waumini wenye kumuogopa Mwenyezi Mungu, «Ni kitu gani Alichokiteremsha Mwenyezi Mungu kwa Nabii Muhammad, rehema na amani zimshukie?» wanasema, «Mwenyezi Mungu Amemteremshia wema na uongofu.» Wale waliomuamini Mwenyezi Mungu na Mtume Wake hapa duniani na wakawalingania waja wa Mwenyezi Mungu kwenye Imani na matendo mema, watapata heshima kubwa ya kupewa ushindi duniani na riziki kunjufu. Na nyumba ya Akhere ni bora kwao na ni kubwa kuliko vile walivyopewa duniani. Na nyumba yenye neema zaidi ya wale wachamungu wenye kumuogopa Mwenyezi Mungu ni Akhera.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس