أَفَأَمِنَ ٱلَّذِينَ مَكَرُواْ ٱلسَّيِّـَٔاتِ أَن يَخۡسِفَ ٱللَّهُ بِهِمُ ٱلۡأَرۡضَ أَوۡ يَأۡتِيَهُمُ ٱلۡعَذَابُ مِنۡ حَيۡثُ لَا يَشۡعُرُونَ
Je! Wameaminisha wanao fanya vitimbi vya uovu kwamba Mwenyezi Mungu hatawadidimiza katika ardhi, na haitawafika adhabu kutoka wasipo pajua?
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Je, wanajiaminisha wale makafiri wanaopanga vitimbi kwamba Mwenyezi Mungu Hatawadidimiza ndani ya ardhi kama Alivyomfanya Qarun au kwamba adhabu haitawafikia kutoka mahali wasipopadhania na wasipopatarajia
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس