وَإِذَا بُشِّرَ أَحَدُهُم بِٱلۡأُنثَىٰ ظَلَّ وَجۡهُهُۥ مُسۡوَدّٗا وَهُوَ كَظِيمٞ
Na mmoja wao akibashiriwa kwa msichana, uso wake unasawijika, naye kajaa chuki.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Na pindi anapokuja mwenye kumpasha habari mmoja wao ya kuzaliwa mtoto wa kike, uso wake hapohapo unageuka mweusi, kwa kuyachukia aliyoyasikia, na akajawa na hasira na huzuni.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس