يَعۡرِفُونَ نِعۡمَتَ ٱللَّهِ ثُمَّ يُنكِرُونَهَا وَأَكۡثَرُهُمُ ٱلۡكَٰفِرُونَ
Wanazijua neema za Mwenyezi Mungu, kisha wanazikanusha; na wengi wao ni makafiri.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Washirikina hawa wazijua neema za Mwenyezi Mungu juu yao za kutumilizwa Muhammad, rehema ya Mwenyezi Mungu na amani zimshukie, kwao, kisha wanaukanusha utume wake. Na wengi wa watu wake ni wale wanaoukanusha utume wake na sio wanaoukubali.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس