وَمَن كَانَ فِي هَٰذِهِۦٓ أَعۡمَىٰ فَهُوَ فِي ٱلۡأٓخِرَةِ أَعۡمَىٰ وَأَضَلُّ سَبِيلٗا
Na aliye kuwa hapa kipofu, basi atakuwa kipofu Akhera, na atakuwa aliye ipotea zaidi Njia.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Na aliyekuwa kipofu wa moyo, katika ulimwengu huu, wa kutoziona dalili za uweza wa Mwenyezi Mungu, asiyaamini yale aliyokuja nayo Mtume Muhammad, rehema na amani zimshukiye, basi yeye, Siku ya Kiyama, atakuwa kipofu zaidi wa kutoiona njia ya Peponi na atapotea zaidi njia ya uongofu na usawa.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس