فَلَمَّا جَآءَهُم بِـَٔايَٰتِنَآ إِذَا هُم مِّنۡهَا يَضۡحَكُونَ
Lakini alipo wajia na Ishara zetu wakaingia kuzicheka.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Na alipowajia na dalili zilizo wazi zenye kuonyesha ukweli wake katika ulinganizi wake, hapo Fir’awn na viongozi wa utawala wake wakawa wanazicheka zile hoja na mazingatio alivyokuja navyo Mūsā.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس