وَنَادَوۡاْ يَٰمَٰلِكُ لِيَقۡضِ عَلَيۡنَا رَبُّكَۖ قَالَ إِنَّكُم مَّـٰكِثُونَ
Nao watapiga kelele waseme: Ewe Malik! Na atufishe Mola wako Mlezi! Naye aseme: Hakika nyinyi mtakaa humo humo!
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Na hao wahalifu waliomkanusha Mwenyezi Mungu, baada ya Mwenyezi Mungu kuwatia kwenye moto wa jahanamu, watamwita Malik, mshika hazina za Moto kwa kusema, «Ewe Malik! Basi na Atufishe Mola wako, tupate kupumzika na haya tuliyonayo,” Hapo Malik awajibu, «Nyinyi ni wenye kukaa, hamna kutoka Motoni na hamna makimbilio ya kujiepusha nao.”
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس