ترجمة معاني سورة العلق باللغة السواحلية من كتاب Ali Muhsin Al - Swahili translation
ﰡ
آية رقم 1
ﮕﮖﮗﮘﮙ
ﮚ
Al'Alak
Soma kwa jina la Mola wako Mlezi aliye umba,
آية رقم 2
ﮛﮜﮝﮞ
ﮟ
Amemuumba binaadamu kwa tone la damu,
آية رقم 3
ﮠﮡﮢ
ﮣ
Soma! Na Mola wako Mlezi ni Karimu kushinda wote!
آية رقم 4
ﮤﮥﮦ
ﮧ
Ambaye amefundisha kwa kalamu.
آية رقم 5
ﮨﮩﮪﮫﮬ
ﮭ
Kamfundisha mtu aliyo kuwa hayajui.
آية رقم 6
ﮮﮯﮰﮱ
ﯓ
Kwani! Hakika mtu bila ya shaka huwa jeuri
آية رقم 7
ﯔﯕﯖ
ﯗ
Akijiona katajirika.
آية رقم 8
ﯘﯙﯚﯛ
ﯜ
Hakika kwa Mola wako Mlezi ndio marejeo.
آية رقم 9
ﯝﯞﯟ
ﯠ
Umemwona yule anaye mkataza
آية رقم 10
ﯡﯢﯣ
ﯤ
Mja anapo sali?
آية رقم 11
ﯥﯦﯧﯨﯩ
ﯪ
Umeona kama yeye yuko juu ya uwongofu?
آية رقم 12
ﯫﯬﯭ
ﯮ
Au anaamrisha uchamngu?
آية رقم 13
ﭑﭒﭓﭔ
ﭕ
Umeona kama yeye akikanusha na anarudi nyuma?
آية رقم 14
ﭖﭗﭘﭙﭚ
ﭛ
Hajui ya kwamba Mwenyezi Mungu anaona?
آية رقم 15
ﭜﭝﭞﭟﭠﭡ
ﭢ
Kwani! Kama haachi, tutamkokota kwa shungi la nywele!
آية رقم 16
ﭣﭤﭥ
ﭦ
Shungi la uwongo, lenye makosa!
آية رقم 17
ﭧﭨ
ﭩ
Basi na awaite wenzake!
آية رقم 18
ﭪﭫ
ﭬ
Nasi tutawaita Mazabania!
آية رقم 19
ﭭﭮﭯﭰﭱﭲ
ﭳ
Hasha! Usimt'ii! Nawe sujudu na ujongee!
تقدم القراءة