وَيَخِرُّونَ لِلۡأَذۡقَانِ يَبۡكُونَ وَيَزِيدُهُمۡ خُشُوعٗا۩
Na huanguka kifudifudi na huku wanalia, na inawazidisha unyenyekevu.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Na hapo hawa wanapomoka hali ya kusujudu kwa nyuso zao, huku wakilia kwa kuathirika na mawaidha ya Qur’ani. Na kule kuisikia Qur’ani na mawaidha yake kunawafanya wazidi kuinyenyekea amri ya Mwenyezi Mungu na kuunyenyekea uweza Wake mkubwa.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس