تِلۡكَ ءَايَٰتُ ٱللَّهِ نَتۡلُوهَا عَلَيۡكَ بِٱلۡحَقِّۗ وَمَا ٱللَّهُ يُرِيدُ ظُلۡمٗا لِّلۡعَٰلَمِينَ
Hizi ni Aya za Mwenyezi Mungu tunakusomea kwa haki. Na Mwenyezi Mungu hataki kuwadhulumu walimwengu.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Hizi ni aya za Mwenyezi Mungu na hoja Zake zenye kung’ara, tunakusomea na kukusimulia, ewe Mtume, kwa ukweli na yakini. Na Mwenyezi Mungu Hakuwa ni mweye kumdhulumu yoyote katika viumbe Wake wala si mwenye kupunguza chochote katika vitendo vyao, kwani Yeye ni Hakimu Mwenye uadilifu Asiyedhulumu.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس