إِنَّ ٱلَّذِينَ كَفَرُواْ لَن تُغۡنِيَ عَنۡهُمۡ أَمۡوَٰلُهُمۡ وَلَآ أَوۡلَٰدُهُم مِّنَ ٱللَّهِ شَيۡـٔٗاۖ وَأُوْلَـٰٓئِكَ أَصۡحَٰبُ ٱلنَّارِۖ هُمۡ فِيهَا خَٰلِدُونَ
Hakika wale walio kufuru hazitawafaa kitu mali zao wala watoto wao mbele ya Mwenyezi Mungu. Na hao ndio watu wa Motoni - humo watadumu.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Hakikia wale waliozikufuru aya za Mwenyezi Mungu na wakawakanusha Mitume Wake, mali yao wala watoto wao havitawatetea wao kivyovyote wasipatwe na adhabu ya Mwenyezi Mungu, duniani wala Akhera. Hao ni watu wa Motoni watakaodumu humo pasi na kutoka.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس