۞وَسَارِعُوٓاْ إِلَىٰ مَغۡفِرَةٖ مِّن رَّبِّكُمۡ وَجَنَّةٍ عَرۡضُهَا ٱلسَّمَٰوَٰتُ وَٱلۡأَرۡضُ أُعِدَّتۡ لِلۡمُتَّقِينَ
Na yakimbilieni maghfira ya Mola wenu Mlezi, na Pepo ambayo upana wake ni mbingu na ardhi, iliyo wekwa tayari kwa wachamngu,
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Na kimbilieni, kwa kumtii kwenu Mwenyezi Mungu na Mtume wake, ili kupata msamaha mkubwa utokao kwa Mola wenu na mpate Pepo kunjufu, upana wake ni sawa na mbingu na ardhi, Ameiandaa Mweyezi Mungu kwa wachamungu.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس