إِنَّمَا ذَٰلِكُمُ ٱلشَّيۡطَٰنُ يُخَوِّفُ أَوۡلِيَآءَهُۥ فَلَا تَخَافُوهُمۡ وَخَافُونِ إِن كُنتُم مُّؤۡمِنِينَ
Hakika huyo ni Shet'ani anawatia khofu marafiki zake, basi msiwaogope, bali niogopeni Mimi mkiwa nyinyi ni Waumini.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Hakika anyewazorotesha nyinyi katika hilo ni Shetani. Amewajia kuwafanya nyinyi muwaogope wasaidizi wake. Basi msiwaogope washirikina, kwani wao ni wanyonge, hakuna mwenye kuwanusuru. Niogopeni mimi kwa kuelekea kwangu kwa utiifu, iwapo nyinyi kweli mnaniamini na mnamfuata Mtume wangu.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس