يَـٰٓأَيُّهَا ٱلَّذِينَ ءَامَنُواْ ٱصۡبِرُواْ وَصَابِرُواْ وَرَابِطُواْ وَٱتَّقُواْ ٱللَّهَ لَعَلَّكُمۡ تُفۡلِحُونَ
Enyi mlio amini! Subirini, na shindaneni kusubiri, na kuweni macho, na mcheni Mwenyezi Mungu, ili mpate kufanikiwa.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Enyi mliomuamini Mwenyezi Mungu na Mtume Wake na mkafuata sheria Zake kivitendo, kuweni na subira juu ya kumtii Mola wenu na juu yaliyowashukia ya madhara na shida, na washindeni maadui zenu katika kusubiri wasipate kuwa wasubirifu zaidi kuliko nyinyi, na simameni wima katika kumpiga vita adui yangu na adui yenu. Na muogopeni Mwenyezi Mungu, katika hali zenu zote, ili mfaulu kupata radhi Zake ulimwenguni na Akhera.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس