إِنَّ ٱلَّذِينَ يَكۡفُرُونَ بِـَٔايَٰتِ ٱللَّهِ وَيَقۡتُلُونَ ٱلنَّبِيِّـۧنَ بِغَيۡرِ حَقّٖ وَيَقۡتُلُونَ ٱلَّذِينَ يَأۡمُرُونَ بِٱلۡقِسۡطِ مِنَ ٱلنَّاسِ فَبَشِّرۡهُم بِعَذَابٍ أَلِيمٍ
Hakika wanao zikataa Ishara za Mwenyezi Mungu, na wakawauwa Manabii pasipo haki, na wakawauwa watu waamrishao Haki wabashirie adhabu kali.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Hakika wale wanaozikanusha dalili zilizo wazi na yale waliokuja nayo Mitume, wakawaua Manabii kwa udhalimu bila haki yoyote, na wakawaua wale ambao wanaamrisha uadilifu na kufuata njia ya Mitume, wape bishara ya adhabu yenye uchungu.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس