قُلۡ إِن كُنتُمۡ تُحِبُّونَ ٱللَّهَ فَٱتَّبِعُونِي يُحۡبِبۡكُمُ ٱللَّهُ وَيَغۡفِرۡ لَكُمۡ ذُنُوبَكُمۡۚ وَٱللَّهُ غَفُورٞ رَّحِيمٞ
Sema: Ikiwa nyinyi mnampenda Mwenyezi Mungu basi nifuateni mimi, Mwenyezi Mungu atakupendeni na atakufutieni madhambi yenu. Na Mwenyezi Mungu ni Mwenye kufuta madhambi na Mwenye kurehemu.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Sema, ewe Mtume, «Ikiwa nyinyi munampenda Mwenyezi Mungu kikweli, nifuateni mimi na kuniaminini, ndani na nje, ndipo Mwenyezi Mungu Atawapenda na Atawasamehe madhambi yenu.Kwani Mwenyezi Mungu ni Mwingi wa kusamehe madhambi ya waja Wake Waumini, ni Mwingi wa rehema kwao.» Aya hii tukufu yamhukumu kila anayedai kumpenda Mwenyezi Mungu, Aliyetukuka, na akawa hamfuati Nabii Wake Muhammad, rehema ya Mwenyezi Mungu na amani zimshukie, kama ipasavyo kufuatwa, na wala hamtii katika maamrisho yake na makatazo yake, kuwa yeye ni mrongo katika madai yake mpaka amfuate Mtume , rehema ya Mwenyezi Mungu na amani zimshukie, kama ipasavyo kufuatwa.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس