يَـٰٓأَهۡلَ ٱلۡكِتَٰبِ لِمَ تَلۡبِسُونَ ٱلۡحَقَّ بِٱلۡبَٰطِلِ وَتَكۡتُمُونَ ٱلۡحَقَّ وَأَنتُمۡ تَعۡلَمُونَ
Enyi Watu wa Kitabu! Mbona kweli mnaivisha uwongo, na kweli mnaificha na hali mnajua?
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Enyi watu wa Taurati na Injili! Kwa nini nyinyi mnachanganya haki iliyo ndani ya vitabu vyenu, kwa yale ya ubatilifu mliyoyapotosha na kuya kwa mikono yenu, na kuzificha kwenu sifa za Muhammad , rehema ya Mwenyezi Mungu na amani zimshukie, ziliomo ndani ya vitabu hivyo viwili na (kuficha kwenu) kwamba Dini yake ndiyo ya haki, na hali nyinyi mnajua hilo?
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس