وَلَا يَأۡمُرَكُمۡ أَن تَتَّخِذُواْ ٱلۡمَلَـٰٓئِكَةَ وَٱلنَّبِيِّـۧنَ أَرۡبَابًاۚ أَيَأۡمُرُكُم بِٱلۡكُفۡرِ بَعۡدَ إِذۡ أَنتُم مُّسۡلِمُونَ
Wala hatakuamrisheni kuwafanya Malaika na Manabii kuwa ni miungu. Je, atakuamrisheni ukafiri baada ya kuwa nyinyi Waislamu?
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Na haikuwa kwa yoyote katika wao awaamrishe nyinyi kuwafanya Malaika na Mitume ni wola wasiokuwa Mwenyezi Mungu ambao nyinyi mnawaabudu. Je, inaingia akilini, enyi watu, yeye awaamrishe kumkanusha Mwenyezi Mungu baada ya kufuata kwenu amri yake?
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس