هَلۡ يَنظُرُونَ إِلَّآ أَن تَأۡتِيَهُمُ ٱلۡمَلَـٰٓئِكَةُ أَوۡ يَأۡتِيَ أَمۡرُ رَبِّكَۚ كَذَٰلِكَ فَعَلَ ٱلَّذِينَ مِن قَبۡلِهِمۡۚ وَمَا ظَلَمَهُمُ ٱللَّهُ وَلَٰكِن كَانُوٓاْ أَنفُسَهُمۡ يَظۡلِمُونَ
Wanangojea jengine hawa ila Malaika wawafikie, au iwafikie amri ya Mola wako Mlezi? Kama hivyo walitenda walio kuwa kabla yao. Na Mwenyezi Mungu hakuwadhulumu, lakini walijidhulumu wenyewe.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Washirikina hawangojei isipokuwa wajiwe na Malaika wazichukue roho zao wakiwa katika hali ya ukafiri, au ije ya amri ya Mwenyewzi Mungu na adhabu ya haraka ya kuwaangamiza. Na kama walivyokanusha hawa, walikanusha makafiri kabla yao, Mwenyezi Mungu Akawaangamiza. Wala Mwenyezi Mungu Hakuwadhulumu kwa kuwaangamiza na kuwaadhibu, lakini wao ndio waliokuwa wakizidhulumu nafsi zao kwa mambo yaliyowafanya wastahili kuadhibiwa.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس