وَقُلۡ جَآءَ ٱلۡحَقُّ وَزَهَقَ ٱلۡبَٰطِلُۚ إِنَّ ٱلۡبَٰطِلَ كَانَ زَهُوقٗا
Na sema: Kweli imefika, na uwongo umetoweka. Hakika uwongo lazima utoweke!
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Na useme, ewe Mtume, kuwaambia washirikina, «Uislamu umekuja na ushirikina umeondoka. Kwani ubatilifu hauna kusalia wala kujikita, na ukweli ndio wenye kuimarika na kusalia ambao hauondoki.»
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس