وَكَيۡفَ تَكۡفُرُونَ وَأَنتُمۡ تُتۡلَىٰ عَلَيۡكُمۡ ءَايَٰتُ ٱللَّهِ وَفِيكُمۡ رَسُولُهُۥۗ وَمَن يَعۡتَصِم بِٱللَّهِ فَقَدۡ هُدِيَ إِلَىٰ صِرَٰطٖ مُّسۡتَقِيمٖ
Na vipi mkufuru hali nyinyi mnasomewa Aya za Mwenyezi Mungu na Mtume yuko kati yenu? Na mwenye kushikamana na Mwenyezi Mungu basi huyo ameongozwa kwenye Njia Iliyo Nyooka.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Na vipi mtamkufuru Mwenyezi Mungu, enyi Waumini, ilhali mnasomewa aya za Qur’ani, na Mtume wa Mwenyezi Mungu, Muhammad , rehema ya Mwenyezi Mungu na amani zimshukie, anazifikisha aya hizo kwenu? Na yoyote atakayetegemea kwa Mwenyezi Mungu, akashikamana na Qur’ani na mafundisho ya Mtume (Sunnah), basi huyo ameafikiwa kufuata njia iliyo wazi na mpango uliolingana sawa.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس