قَدۡ خَلَتۡ مِن قَبۡلِكُمۡ سُنَنٞ فَسِيرُواْ فِي ٱلۡأَرۡضِ فَٱنظُرُواْ كَيۡفَ كَانَ عَٰقِبَةُ ٱلۡمُكَذِّبِينَ
Kabla yenu zimepita nyendo nyingi; basi tembeeni katika ulimwengu muangalie vipi ulikuwa mwisho wa wanao kanusha.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Mwenyezi Mungu Anawazungumzia Waumini walipopatwa na mikasa siku ya vita vya Uhud kwa kuwaliwaza kwamba wamepita kabla yao ummah wengi ambao waumini kati yao walitahiniwa kwa kupigana na makafiri na ukawa ushindi ni wao. Basi, tembeeni katika ardhi mkizingatia yale yaliyowafika wale waliomkanusha Mwenyezi Mungu na na Mtume Wake.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس