يَـٰٓأَيُّهَا ٱلَّذِينَ ءَامَنُوٓاْ إِن تُطِيعُواْ ٱلَّذِينَ كَفَرُواْ يَرُدُّوكُمۡ عَلَىٰٓ أَعۡقَٰبِكُمۡ فَتَنقَلِبُواْ خَٰسِرِينَ
Enyi mlio amini! Ikiwa mtawat'ii walio kufuru watakurudisheni nyuma, na hapo mtageuka kuwa wenye kukhasiri.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Enyi mliomuamini Mwenyezi Mungu na Mtume Wake na mkazifuata sheria Zake kivitendo! Iwapo mtawatii walioukanusha uungu wangu na wasiwaamini Mitume wangu, miongoni mwa Mayahudi, Wanaswara, wanafiki na washirikina, katika yale wanayowaamrisha nyinyi nayo na wanayowakataza nyinyi nayo, watawapoteza njia ya haki na mtaritadi muache dini yenu na mrudi na hasara iliyo wazi na maangamivu ya kikweli.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس