إِن يَنصُرۡكُمُ ٱللَّهُ فَلَا غَالِبَ لَكُمۡۖ وَإِن يَخۡذُلۡكُمۡ فَمَن ذَا ٱلَّذِي يَنصُرُكُم مِّنۢ بَعۡدِهِۦۗ وَعَلَى ٱللَّهِ فَلۡيَتَوَكَّلِ ٱلۡمُؤۡمِنُونَ
Akikunusuruni Mwenyezi Mungu hapana wa kukushindeni, na akikutupeni ni nani, basi, baada yake Yeye ataye kunusuruni? Na Waumini wamtegemee Mwenyezi Mungu tu.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Iwapo Mwenyezi Mungu Atawapa msaada na nusura Yake, hapana yoyota awezaye kuwashinda. Na iwapo Atawaacha kuwasaidia na kuwanusuru, basi ni nani awezaye kuwanusuru nyinyi baada ya Yeye kuacha kuwanusuru? Na kwa Mwenyezi Mungu, Peke Yake, nawajitegemeze Waumini.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس