۞يَسۡتَبۡشِرُونَ بِنِعۡمَةٖ مِّنَ ٱللَّهِ وَفَضۡلٖ وَأَنَّ ٱللَّهَ لَا يُضِيعُ أَجۡرَ ٱلۡمُؤۡمِنِينَ
Wanashangilia neema na fadhila za Mwenyezi Mungu, na ya kwamba Mwenyezi Mungu hapotezi ujira wa Waumini,
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Hakika wao watakuwa wamejawa na furaha kwa neema za Mwenyezi Mungu na vipawa Vyake vingi na hakika Mwenyezi Mungu Hayapotezi malipo ya ya wenye kumuamini, bali Anayakuza na kuyaongeza kwa fadhila Zake.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس