لَّقَدۡ سَمِعَ ٱللَّهُ قَوۡلَ ٱلَّذِينَ قَالُوٓاْ إِنَّ ٱللَّهَ فَقِيرٞ وَنَحۡنُ أَغۡنِيَآءُۘ سَنَكۡتُبُ مَا قَالُواْ وَقَتۡلَهُمُ ٱلۡأَنۢبِيَآءَ بِغَيۡرِ حَقّٖ وَنَقُولُ ذُوقُواْ عَذَابَ ٱلۡحَرِيقِ
Mwenyezi Mungu amekwisha sikia kauli ya walio sema: Mwenyezi Mungu ni masikini, na sisi ni matajiri. Tumeyaandika waliyo yasema, na pia kuwauwa kwao Manabii bila ya haki, na tutawaambia Siku ya Kiyama: Onjeni adhabu ya kuungua.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Hakika Amelisikia Mwenyezi Mungu neno la Mayahudi ambao walisema, «Mwenyezi Mungu ni muhitji kwetu, Anatutaka tumkopeshe mali, na sisi ni matajiri.» Tutaliandika neno hili walilolisema na tutaandika kwamba wao wako radhi na yale yaliyofanyika ya kwamba mababa zao waliwaua Manabii wa Mwenyezi Mungu kwa dhuluma na uadui. Tutawaadhibu kwa hilo huko Akhera na tutawaambia, nao wamo Motoni waadhibiwa, «Ionjeni adhabu ya Moto unaounguza.»
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس