كُلُّ نَفۡسٖ ذَآئِقَةُ ٱلۡمَوۡتِۗ وَإِنَّمَا تُوَفَّوۡنَ أُجُورَكُمۡ يَوۡمَ ٱلۡقِيَٰمَةِۖ فَمَن زُحۡزِحَ عَنِ ٱلنَّارِ وَأُدۡخِلَ ٱلۡجَنَّةَ فَقَدۡ فَازَۗ وَمَا ٱلۡحَيَوٰةُ ٱلدُّنۡيَآ إِلَّا مَتَٰعُ ٱلۡغُرُورِ
Kila nafsi itaonja mauti. Na bila ya shaka mtapewa ujira wenu kaamili Siku ya Kiyama. Na atakaye epushwa na Moto na akatiwa Peponi basi huyo amefuzu. Na maisha ya dunia si kitu ila ni starehe ya udanganyifu.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Nafsi yoyote, hapana budi, itayaonja mauti. Na kwa hivyo, viumbe wote watarudi kwa Mola wao ili Awahesabu. Na kwa hakika mtalipwa malipo yenu kikamilifu Siku ya Kiyama juu ya vitendo vyenu bila kupunguziwa. Basi yule ambaye Mola wake Atamkirimu, Akamuokoa na Moto na Akamtia Peponi, huyo atakuwa amepata upeo wa ayatakayo. Na hayakuwa maisha ya duniani isipokuwa ni kiliwazo cha kuondoka. Basi msighurike nayo.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس