إِنَّ فِي خَلۡقِ ٱلسَّمَٰوَٰتِ وَٱلۡأَرۡضِ وَٱخۡتِلَٰفِ ٱلَّيۡلِ وَٱلنَّهَارِ لَأٓيَٰتٖ لِّأُوْلِي ٱلۡأَلۡبَٰبِ
Hakika katika kuumbwa mbingu na ardhi na kukhitalifiana usiku na mchana ziko Ishara kwa wenye akili,
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Hakika, katika kuziumba mbingu na ardhi, pasi na kuwa na mfano uliotangulia, na katika kufuatana usiku na mchana na kutafautiana kwao, urefu na ufupi, pana dalili na hoja kubwa zinazobainisha upweke wa Mwenyezi Mungu kwa walio na akili timamu.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس