رَبَّنَآ إِنَّكَ مَن تُدۡخِلِ ٱلنَّارَ فَقَدۡ أَخۡزَيۡتَهُۥۖ وَمَا لِلظَّـٰلِمِينَ مِنۡ أَنصَارٖ
Mola wetu Mlezi! Hakika unaye mtia Motoni umemhizi; na walio dhulumu hawana wasaidizi.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
«Ewe Mola wetu! Tuokue na Moto, kwani hakika Wewe, ewe Mwenyezi Mungu, yoyote Utakayemuingiza Motoni kwa madhambi yake, ushamfedhehesha na kumtweza. Na watenda madhambi, wanaozidhulumu nafsi zao, hawatakuwa na yoyote wa kuwatetea wasipate adhabu ya Mwenyezi Mungu Siku ya Kiyama.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس