قُلۡ أَطِيعُواْ ٱللَّهَ وَٱلرَّسُولَۖ فَإِن تَوَلَّوۡاْ فَإِنَّ ٱللَّهَ لَا يُحِبُّ ٱلۡكَٰفِرِينَ
Sema: Mt'iini Mwenyezi Mungu na Mtume. Na wakigeuka basi Mwenyezi Mungu hawapendi makafiri.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Sema, ewe Mtume, «Mtiini Mwenyezi Mungu kwa kufuata Kitabu Chake, na mtiini Mtume kwa kufuata mwenendo wake wakati wa uhai wake na baada ya kufa kwake.Wakiwa watakupa mgongo na kukamaa kwenye ukafiri na upotevu walionao, wao hawatakuwa wanastahili mapenzi ya Mwenyezi Mungu. Kwani Mwenyezi Mungu Hawapendi makafiri.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس