ذُرِّيَّةَۢ بَعۡضُهَا مِنۢ بَعۡضٖۗ وَٱللَّهُ سَمِيعٌ عَلِيمٌ
Ni wazao wao kwa wao; na Mwenyezi Mungu ni Mwenye kusikia na Mwenye kujua.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Manabii hawa na Mitume ni mlolongo wa usafi wenye kuungana katika kumtakasa Mwenyezi Munguna, kumpwekesha na kutenda vitendo vinavyoambatana na wahyi Wake. Na Mwenyezi Mungu ni Mwenye kuyasikia maneno ya waja Wake, ni Mjuzi wa vitendo vyao na Atawalipa kwavyo.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس